Kuhusu TAG
Tanzania Assemblies of God (TAG) ilisajiliwa tarehe 21/10/1981 chini ya sheria ya Societies Ordinance ya mwaka 1954 na kupewa namba ya usajili SO. 6246
soma zaidiMakao Makuu
Makao makuu ya kanisa pamoja na ofisi ya idara yetu zilihamia Rasmi Dodoma mnamo tarehe 01/11/2021, hivyo huduma zetu zote zinatolewa mkoani Dodoma karibu katika ofisi zetu.
Bezaleli
Kanisa letu lina mfumo wa kidigitali uitwao Bezaleli, ili kuweza kuingia kwenye mfumo wetu tafadhali Bofya Hapa
Kuhusu Idara ya Elimu
Idara ya Elimu ni mojawapo ya Idara kumi na moja za Kanisa la Tanzania Assemblies of God, iliyoanzishwa kwa ajili ya kufanikisha maono na malengo yake. Kusudi la kuwepo kwa Idara ni kupanga, kuratibu, na kusimamia utekelezaji ili kuwa na watumishi waliondaliwa vema kiroho na kitaaluma, wenye kuakisi tabia na mtazamo wa Yesu katika maisha na huduma. Idara inatoa mafunzo kwa watumishi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God na Madhehebu mbalimbali ya Kipentekoste tunayokubaliana nayo kiimani ndani na nje ya nchi.Idara ya Elimu ina Vyuo vya Biblia tisa. Vyuo vya bweni saba, kimoja cha kutwa, na kimoja huria. Ili kuharakisha kazi ya kuivuna Tanzania...
soma zaidiLengo letu Kuu
Kuratibu mafunzo yatolewayo katika Vyuo vya Biblia, Vyuo vya Kupanda Makanisa na Mafunzo Endelevu ili kutoa elimu bora kwa lengo la kuwa na watumishi wenye uwezo na maadili ya kibiblia. Kuandaa mtaala wenye sifa zinazohakikisha kwamba elimu inayotolewa inakidhi hitaji la Kanisa la TAG na aina ya cheti kinachotolewa kwa mhitimu.
Shuhuda
Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu.
"Bwana na ainue viongozi kwa mataifa yetu ambao wataitikia kwa usahihi mahitaji yake ya uaminifu.
Waefeso 2:10 “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.