Miaka 13 ya Moto wa Uamsho
Tunamtaka Bwana na Nguvu zake

Kuandaa watumishi wa Mungu waliojawa na Roho Mtakatifu ili kuyafikia Mataifa
Kauli Lengo
Idara ya Elimu ni mojawapo ya Idara kumi za Kanisa la TAG
Kusudi la kuwepo kwa Idara ni kupanga, kuratibu, na kusimamia utekelezaji ili kuwa na watumishi waliondaliwa vema kiroho na kitaaluma, wenye kuakisi tabia na mtazamo wa Yesu katika maisha na huduma. Idara inatoa mafunzo kwa watumishi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God na Madhehebu mbalimbali ya Kipentekoste tunayokubaliana nayo kiimani ndani na nje ya nchi.


Watumishi wa Idara ya Elimu Makao Makuu

Mch. Jonas Petro Mkoba
Mkurugenzi Mkuu

Mch. Gerald Ole-Nguyaine
Makamu Mkurugenzi

Mch. Joyce Musembe
Katibu Mkuu

Mr. Tadei Mbuta
Mtunza Hazina

Kusudi kuu
Idara ya Elimu ipo ili kupanga, kuratibu na kusimamia utekelezaji wa maono na makusudi ya kuwepo kwake, kama inavyoainishwa kwenye katiba ya kanisa la Tanzania Assemblies of God.
Maono
Kuwa na watumishi waliondaliwa vema kiroho na kitaaluma ili kuakisi tabia na mtazamo wa Yesu katika maisha na huduma
Vyuo vyetu






Maadili ya Msingi
Idara ya Elimu ya kanisa la Tanzania Assemblies of God ina Maadili ya Msingi yapatayo 6
Utakatifu na uadilifu
Uwajibikaji
Ibada
Uaminifu kwa Biblia
Kufanya kazi kama timu
Ufanisi

Vyuo vyetu
Idara ya Elimu ina Vyuo vya Biblia vinane. Vyuo vya bweni sita, kimoja cha kutwa, na kimoja huria.
Kila Kanda ina Chuo Mama kama ifuatavyo: Kanda ya Kusini Mashariki South-Eastern Bible College, Mtama, Lindi. Kanda ya Kusini Southern Bible College, Mbeya. Kanda ya Kati Central Bible Collge, Dodoma. Kanda ya Ziwa Lake Victoria Bible College, Mwanza. Kanda ya Kaskazini Northern Bible College, Arusha. Kanda ya Magharibi Western Bible College, Ilolanguru, Tabora. Kanda ya Kaskazini Mashariki Global Harvest Bible College, Dar –Es – Salaam, na Global University ambacho kinaendesha mafunzo yake nchi nzima.